Kuna mzee mmoja alibahatika kupata mtoto mmoja tu tena wa kike. Yule mzee alikuwa anampenda sana binti yake kiasi alidiriki kumpa kila alichokihitaji licha ya ufukara uliokuwa unamtaabisaha sana huyo mzee.
Siku moja yule binti akiwa na umri wa miaka 15, baba yake akagundua kuwa binti yake ni mjamzito. Akamfokea sana binti yake na akamwamuru ampeleke kwa mwanaume aliyempa hiyo mimba!
Walipofika kwa huyo mla vya watu tena ambavyo havijakomaa kwa hasira huku akitweta mpaka povu likawa lamtoka mdomoni mazungumuzo yao yalikuwa hivi;
Mzee: Wewe unajifanya kidume sana mpaka ukamtia mimba mwanafunzi sio? Mwaka huu nakufunga mshenzi mkubwa wewe! Hii mimba ni ya nani?
Kijana: Ni kweli nimempa ujauzito binti yako, ila akizaa dume nitampa nitampa daladala kumi, sheli tatu na milioni 50 kama mtaji! Akizaa binti, nitakupa supermarket 3, mashamba makubwa sita na milioni 40!
Binti: Mimba ikitoka je?
Mzee: Nyamaza mpumbavu wewe, si atakupa nyingine!
Tafakari
**********



