Kuna kila sababu ya kumheshimu sana mzazi wako maana wazazi hupitia shida nyingi sana ili kuhakikisha tu wanawalinda watoto wao. Hii si kwa wanadamu pekee kwani hata viumbe wengine wana upendo wa dhati sana kwa watoto wao!
Suala la kuzaa kwa mwanamke wa kiafrika hivi sasa limekuwa ni ugonjwa. Hii ni tofauti na dhana nzima iliyokuwepo zamani kwani kwa sasa maisha ya mama mjamzito yapo hatarini zaidi kuliko hapo awali.
Huwa linakuwa ni jambo la kumshukuru MUNGU sana iwapo mama mjamzito akabahatika kujifungua salama salimini. Kama madhara hayatamfika mtoto basi mama au wote kwa pamoja! Inawezekana kukawepo sababu ambazo zinaweza kuelezwa kitaalam lakini jambo la msingi ni kumshukuru sana mama yako kwa kukuzaa salama!
Video ifuatayo inaonyesha namna mwanamke mjamzito anavyofanyiwa upasuaji kwa ajili ya kumtoa mtoto baada ya njia za kawaida za uzazi kukwama. Video hii ndio iliyonifanya nikukumbushe kwamba unapaswa kumheshimu sana mama yako siku zote za uhai wako pasipo kujali ana hali gani!
Angalia Video Hii Hapa Chini

