Home Vichekesho Mahakama Zetu Nazo Haziishi Mikasa, Bubu Aitwa Kutoa Ushahidi!

Mahakama Zetu Nazo Haziishi Mikasa, Bubu Aitwa Kutoa Ushahidi!

408
0

Mahakamani

Katika mahakama moja kulikuwa na kesi moja mbaya sana ya ubakaji iliyokuwa inamkabiri jamaa mmoja. Shahidi pekee wa kesi hiyo alikuwa ni bubu. Bubu huyo ndiye aliyeushuhudia mchezo wa ubakaji mwanzo mpaka mwisho. Njemba hilo lililofanya ubakaji huo lilimpuuza huyo bubu kwa kukuwa lilikuwa linajua hawezi kuongea.

Lakini kwa ugumu vivyo hivyo yule bubu alikimbia hadi kwao na kutoa taarifa ya tukio hilo. Watu wakajikusanya na kwenda kushuhudia ila kwa bahati mbaya walikuta mbakaji huyo kashaondoka na kamwacha mhanga wa ubakaji akilalama kwa maumivu.


Upelelezi ulifanyika na yule mbakaji akakamatwa na kufikishwa mahakamani. Yule bubu alikuwa ni shahidi mhimu sana katika ile kesi japo alikuwa hawezi kuongea. Ulipofika wakati wa kutoa ushahidi, yule bubu akapanda kizimbani ili atoe ushahidi wake. Hakimu alianza kwa kumwuliza;

Hakimu: Jina lako nani?

Katika hali ya kushangaza yule bubu akashika koo na  uume wake. Hakimu akawa haelewi kitu akarudia mara tatu kumwuliza jina lake ni nani na bubu alifanya vivyo hivyo mara zote. Ikabidi atafutwe MKALIMANI ili asaidia kutoa tafsiri. Alipoulizwa nini maana ya ile Ishara, mkalimani akasema;

Mkalimani: Kasema anaitwa ‘KOMBO’!

Hakimu akachoka!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here