Mwanaume mmoja nchini Kenya alizua kioja cha mwaka pale alipompiga mkewe licha ya yeye kufumaniwa na mkewe. Jamaa huyo ambaye alikuwa ameingia kwenye nyumba moja ya wageni na kimada wake huyo kwa ajili ya kujivinjari, ghafla wasamaria wema walimtonya mkewe kuwa anaibiwa!
Mkewe ikamlazimu aende mpaka kwenye hiyo gesti ili akajionee mwenyewe. Baada ya kumgongea mume wake akiwa chumbani na mke wa mtu, mumewe alimwambia akifungua atamwua hivyo yule mama aliamua kusubiri kwa muda ili aone kama mumewe atatoka. Baada ya muda yule mwanaume alitoka mle chumbani na kumkuta mkewe anamsubiri nje na kisha kumwanzishia kichapo pasipokujua kulikuwa na kamera zinamrekodi.
Yule mama ilibidi apinge yowe kwa lengo la kuomba msaada na baadhi ya watu wakaja kumsaidia. Lakini dakika kadhaa baadae yule mwanaume aliingia kwenye gari lake na kimada wake wakatokomea. Inadaiwa mwanaume huyo ameitelekeza familia yake na anaishi na wanawake wengine nje ya nyumba yake.
Video Yake Hii Hapa
**********


Hahahaha ni nouma
Ndo inatakiwa hivyo so ukifumania ujipange
Ndo inatakiwa hivyo so ukifumania ujipange