Kuna kila sababu ya kujivunia uumbaji wa MUNGU! Kila mmoja wetu ameumbwa kwa mfano na mapenzi ya dhati ya MUNGU wetu, hii ni kwa mujibu wa vitabu vitakatifu vya kiimani. Inawezekana kabisa tukakinzana imani lakini kila mmoja akaamini kwamba suala la uumbaji ni la kipekee na linaonyesha ukuu wa MUNGU.
Wapo ambao mara nyingi hujaribu kukosoa uumbaji wa MUNGU kwa kujaribu kujiweka vile macho yao yanawapendeza. Inawezekana kabisa macho yako yakavutiwa na vile unavyodhani wataka kuwa ila kwa upande mwingine ikawa ni kufuru kwa Muumbaji wako!
Siku za hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia mapinduzi makubwa sana ya kimaarifa. Sayansi ya hali ya juu imekuwa ikitumika kwa kila jambo. Aidha mapinduzi haya ya kimaarifa si jambo baya hasa yanapotumika kwa manufaa ya wengi pasipo madhara.
Licha ya uhuru wa kuchagua kuishi vile anavyota, bado mwanadamu anawajibu wa kutambua thamani ya kubakia vile alivyo. Tumekuwa tukiona wimbi la watu wa jinsia moja kuwa na mahusiano ya kingono na imefikia wakati watu wanaamua kubadili jinsia zao ili wawe na maumbile wanayoyataka.
Nimeongea sana, hebu angalia video hii utajua ninachokwambia kina maana gani!
Video Hii Hapa


tafadhali ucweke hiyo