Home Video Je, Uliisikia Hii? | Mama Aolewa Na Mwanae Hapa Hapa Tanzania

Je, Uliisikia Hii? | Mama Aolewa Na Mwanae Hapa Hapa Tanzania

470
0

Tanzania imekuwa ikipata sifa kubwa za kuwa na ushirikina hasa dunia iliposhuhudia mauaji ya mazeruzeru kwa madai kuwa viungo vyao vinaleta utajiri. Tumekuwa tukishuhudia wapiga nondo katika mikoa ya Njombe na Mbeya kwa madai kwamba zile nondo zinazotumika zikitundikiwa nyama katika mabucha, wanauza sana. Haya na mengine mengi yameifanya Tanzania ionekane ni nchi yenye watu wanaoamini sana ushirikina.

Katika hali ya kushangaza kuna mkasa ulijitokeza mwaka huu huko mkoani Ruvuma ambako mama mmoja alikuwa anatembea na mtoto wake wa kumzaa! Inawezekana usinielewe sana lakini huu ndio ukweli kwamba mama huyo alikuwa anatembea na mwanae wa kumzaa na cha kushangaza zaidi yule kijana alikiri kumwoa mama yake.


Mkasa huu uliruka katika kituo cha luninga cha Channel Ten ambapo mkasa huo ulikuwa unahusishwa pia na mambo ya kishirikina. Yamesemwa mengi sana lakini kikubwa shuhudia mkasa huu wewe mwenyewe kwa kuangalia video yake.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here