Matumizi ya simu hakika yana mengi ambayo wengi hawayajui. Na kila mmoja ana mambo yake ambayo anaamini kabisa yatakuwa ni siri yake mpaka mwisho wa uhai wake. Katika mahaba simu zimerahisisha sana mawasiliano. Lakini halii imeongeza upungufu wa uaminifu katika mahusiano kwa sababu imekuwa ni rahisi sana kwa watu kuwasiliana kimahaba pasipo kugundulika. Usimwamini sana demu wako hata kama unamtania!
Nakumbuka zamani zile nikiwa shule ya upili miaka ya 90 nilikuwa na demu wangu! Mimi nilikuwa nasoma mkoa na demu wangu alikuwa Dar! Mawasiliano yalikuwa ni ya barua tu ni ilikuwa inachukua wiki nzima kupata barua niliyokuwa natumiwa na my hun!
Lakini sasa mambo yamebadilika sana, ukishapewa namba ya simu tu, uhakika! Hebu tujadili itakuwa vipi simu zetu zikawa zinasikilizwa na watu wa karibu sana katika maisha yetu?
