Siku moja katika hospitali ya machizi, daktari alimkuta mmoja wa machizi hao akiwa uvunguni mwa gari. Alionekana akilikagua kwa makini sana lile gari. Yule daktari akahisi labda mgonjwa wake wa akili amepona na alikuwa anataka kulitengeneza lile gari. Ikabidi amwite na amwulize alichokuwa anakifanya. Yule chizi baada ya kutoka uvunguni mwa gari mazungumuzo yao yalikuwa hivi,
Daktari: Wewe chizi, ulikuwa unafanya nini huko chini?
Chizi: Nilikuwa nalichunguza kama ni jike au dume.
Daktari: Na umegundua nini?
Chizi: Nimegundua lina ulemavu wa viungo vya uzazi, limezaliwa bila viungo vya uzazi.
Daktari akachoka!!!!!
**********



