Ujio wa Rais Obama nchini Tanzania umekuwa gumzo na ulifanya watu wengi kupagawa kwani kila mmoja alikuwa na hamu sana ya kumwona. Mambo mengi yaliwekwa sawa ikiwa ni pamoja na usafi wa jiji, kuondolewa na machinga mabarabarani na mengineyo mengi mazuri. Hakika Ikulu ilipambwa ikapambika ili mgeni aje aione Tanzania inayopendeza.
