Katika shule moja ya upili maarufu sana ya kibinafsi, ilikuwa ni kawaida kwa wanafunzi wanaofanya vizuri kupewa zawadi kila mwisho wa mwaka. Siku hiyo iliwekwa maalum pia kwa ajili ya wazazi kufika shuleni hapo na kushuhudia watoto wao wakipewa zawadi kulingana na jitihada zao za kimasomo na vipawa mbalimbali. Pia ilikuwa ni fursa ya wazazi kwenda kuwachukua watoto wao na kurejea nao makwao kwani siku hiyo mara zote huwa ndiyo siku ya kufunga shule kutokana na kumaliza mwaka wa masomo kwa kila kidato.
Magembe alikuwa ni mmoja wa wazazi ambao walihudhuria katika tafrija hiyo na akashuhudia utoaji na upokeaji wa zawadi kwa wanafunzi. Magembe hakufurahishwa kabisa na ripoti ya kijana wake kwani alikuwa amefeli sana.
Wakati wakiwa kwenye TAXI wanarejea nyumbani gari ambalo Magembe alikuwa analimiliki aliamua kuvunja ukimya na kumfokea kijana wake na mazungumzo yao yalikuwa hivi,
Magembe: Napoteza pesa zangu bure kabisa, umeona watoto wenzako wenye bidii jinsi wanavyopokea zawadi?
Mtoto: Nimeona! Na wewe baba umeona wazazi wenye bidii jinsi wanavyopaki magari ya kifahari Rangerover, BMW, Benz na Hammer wanapokuja kuwatembelea watoto wao?
…………….Ungekuwa wewe ndio Magembe ungejibu nini? ………………….
**********
Bofya Hapa Kuisoma: Soma Taarifa Hii Inaweza Kubadili Maisha Yako, Mfahamishe Na Mwenzako.




teh teh teh teh! hiyo kali.