Kuna jamaa alienda kumwangallia Obama wakati amekuja kuzuru Tanzania maeneo ya Ubungo na akaokota wallet, na alipofika nyumbani kwake akapiga simu redioni na mazungumuzo yalikuwa hivi;
Jamaa: Naitwa Komesho napiga simu toka Mbagala.
Mtangazaji: Una jipya gani Komesho?
Jamaa: Natangaza kuwa nillipokuwa kwenye msukumano wa kumwona Obama jana Ubungo, nikaokota wallet ndani ina laki 7, kadi ya ATM na kikaratasi chenye namba za siri za kadi ya ATM na kidani cha dhahabu.
Mtangazaji: Kwa hiyo ungependa kumrudishia mwenyewe kama anakusikiliza?
Jamaa: Hapana, napenda kumtumia dedication ya wimbo wa R. Kelly “U SAVED ME” umfikie popote pale alipo!
Jamaa akakata simu!
**********



