Home Vichekesho Baniani Mbaya Kiatu Chake Dawa!!!!

Baniani Mbaya Kiatu Chake Dawa!!!!

1648
0

Mgonjwa

Jamaa mmoja alipatwa na maradhi ya ghafla na akawa anahisi kufa kufa! Ile hofu ya kifo ilipomzidi akamwita mkewe ili atubu dhambi na makosa yake yote aliyokuwa amemfanyia mkewe. Hali hiyo iliashiria hali haikuwa shwari kwani muda wowote mgonjwa angekata roho.

Wakati roho ikikaribia kabisa kuacha mwili wake, jamaa huyo akamshikilia kwa nguvu sana mkewe na kuanza kumwambia:

Jamaa: Mke wangu, natubu mbele zako na za Muumba. Nilifanya dhambi kubwa sana ya kutembea na mama yako, dada yako na mdogo wako!

Mke: (Huku akimnong’oneza kwa upole) Usijali mume wangu, nayafahamu hayo yote! Ndiyo maana nimekupa sumu yaani hapa huna dakika tano utakuwa marehemu!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here