Home Vichekesho Habari Nzuri Na Mbaya

Habari Nzuri Na Mbaya

600
0

Mgonjwa mmoja alimpigia simu daktari wake kumwuliza matokeo ya vipimo alivyokuwa amevipeleka jana yake kwa ajili ya kuijua afya yake iliyokuwa inatetereka. Kama unavyojua, madaktari huwa wanakuwa bize sana na haya yalikuwa ni mazungumuzo yao;


Mgonjwa: Hallo!

Daktari: Hallo!

Mgonjwa: Nimepiga kuulizia matokeo ya vipimo vyangu!

Daktari: Okey, nina habari nzuri na mbaya kuhusu wewe!

Mgonjwa: Anza na habari nzuri.

Daktari: Kutokana na vipimo vyako vinavyoonyesha, una saa 24 tu za kuishi.

Mgonjwa: Hiyo ndio habari nzuri? Hebu na hiyo mbaya niisikie!

Daktari: Habari mbaya ni kwamba, nilisahau kukwambia jana kwamba una saa 24 tu za kuishi!

Mgonjwa aliposikia hivyo akaanguka chini kwa hofu akafa!