Home Mbavu Zangu Vichaa Na Mlango Wa kuchorwa

Vichaa Na Mlango Wa kuchorwa

821
0

Katika hospitali moja ya vichaa kulikuwa na vichaa kadha wa kadha waliokuwa wakipata matibabu ya akili. Daktari wao alikuwa anajitahidi kwa hali na mali kuhakikisha wagonjwa wake wa akili wanapona na kurejea hali yao ya kawaida!

Siku moja aliamua kuwapima ili ajue ni wangapi wanapata unafuu au wamepona. Basi daktari huyo aliamua kuwafungia wale vichaa kwenye chumba kisha akachora picha ya mlango ukutani.

Baada ya kuuchora vizuri akawaambia wale vichaa waende mlangoni akionyesha ule mchoro wa mlango uliopo ukutani. Vichaa wote wakakimbilia pale ukutani na kuanza kusukumana wakigombea kutoka isipokuwa kichaa mmoja alibakia kakaa anawaangalia wenzake. Daktari akahisi labda Yule kichaa kapona na kaona haiwezekani kutoka kwani ule haukuwa mlango bali ulikuwa mchoro ukutani.

Mazungumuzo yao yalikuwa hivi:
Daktari: Wewe mbona umekaa hutaki kutoka nje?
Kichaa: Nawashangaa hao vichaa!
Daktari: Kwa nini wawashangaa?
Kichaa: Naona wanaumizana bure hapo wakati ufunguo wa huo mlango ninao mimi!

**********