Inawezekana liakawa ni jambo la kushangaza sana kulielezea kama si kulishuhudia. Kizazi cha sasa kinakabiliwa na tatizo kubwa sana la kuporomoka kwa maadili. Mfumo wa maisha umeyabadili haya yote na watoto wadogo sana wamekuwa wakifanya mambo makubwa ajabu. Hii ni athari inayotokana na utandawazi uliopelekea mfumo wa TEHAMA kuimalika zaidi hivyo hakuna sehemu utaficha habari.
Asipoisikia kwako baso ataisoma katika mitandao na kwingineko kwingi ambako siku hizi habari huzagaa kama moto wa nyika uwakavyo wakati wa machana wa jua kali. Picha hii inaakisi yale ambayo jamii zetu zinapaswa kujiandaa ili kuwa na watoto wenye makuzi mema!
