MTOTO : Baba kwani mimi nimetoka wapi?
BABA: Dah!! Mwanangu mbona unaniuliza swali gumu hivyo? Ene-Wei, hebu kaa hapo nikuhadithie. Mimi na Mama yako siku moja wakati anatoka kazini. Tulikutana Kituo cha Basi , Mvua kubwa ikaanza kunyesha, ikalazimika tuchelewe saaana kupanda basi.Kwa sababu tulikuwa tumekaa pamoja, nilimwona ameloana sana na mvua na alikuwa akitetemeka baridi. Nilimwonea huruma nikamwachia Jaket langu hapo ndiyo tukaanza kuzoeana.Baada ya miezi mitatu tukaona ni vema tuoane!.Tukawaeleza wazazi wetu wakatukubalia, Harusi ikafanyika tena kubwa saana!! Tukaanza kuishi pamoja. Kwa kifupi ndiyo wewe ukapatikana. Ukikua kidogo utanielewa nina maana gani.
MTOTO: Haya, Ila Mwalimu atanipiga nisipomwambia kesho. Katuambia wote tuwaulize Wazazi wetu tumetoka wapi? Mwalimu wetu kasema yeye Ametoka TABORA !!!????




