Baada ya stori nyingi za Prezida mpya wa Tanzania kutapakaa kila kona ya nyumba za watu, nchi, Afrika Mashariki, Afrika na duniani kote; mama mmoja aliona wivu sana na akawa anakasirishwa jinsi mumewe anavyomsifia sana rais huyo kuliko hata yeye mwenyewe (mkewe). Kuona hivyo yule mwanamke akaamua kupima bahari kwa miguu:
Mke: Mume wangu, siku hizi sikuelewi kabis!
Mume: Kwa nini mke wangu?
Mke: Taarifa ya habari ya saa mbili usiku unaisubiri tangia saa kumi jioni na hutaki tuongee chochote!
Mume: Nataka nijue Magufuli kaibukia wapi leo.
Mke: Sasa mimi na Magufuli nani mhimu?
Mume: Acha kumfananisha magufuli na vitu vya Kipuuzi mkewe wangu! Weee vipi!!!!



