MLEVI NA MCHUNGAJI WAMEKUTANA;
Katika pitapita za mchungaji wa kanisa fulani alikutana na mlevi akiwa na chupa yake ya lubisi kama sio balimi huku anabwabwaja maneno mengi sana peke yake. Mchungaji akaamua kuanzisha mazungumuzo ya kumsaidia kiroho yule mlevi;
MCHUNGAJI: Unakunywa bia!?
MLEVI: Ndio.
MCHUNGAJI: Kwa siku unakunywa bia ngapi!?
MLEVI: Nakunywa bia tano!
MCHUNGAJI: Bia moja bei gani!?
MLEVU: 2500/=
MCHUNGAJI: Ulianza lini kunywa bia!?
MLEVI: Miaka 18 iliyopita!
MCHUNGAJI: Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000??
MLEVI: Ndio!
MCHUNGAJI: Kama ungekuwa unatunza hiyo pesa 10,000/= kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover!?
MLEVI: Samahani, naweza kukuuliza swali!?
MCHUNGAJI: Uliza!
MLEVI: Unakunywa bia!?
MCHUNGAJI: Hapana!
MLEVI: Una miaka mingapi?
MCHUNGAJI: 39
MLEVI:Nionyeshe Range Rover yako!
MCHUNGAJI: (Kimya, anaondoka bila kuaga)
**********




huhuh