Usije Ukajaribu, Mke Wa Mtu Sumu!
Mdada mmoja mke wa mtu alikuwa akisumbuliwa sana na jamaa mmoja aliyekuwa akimtaka kila siku. Hatimaye yule mdada akamwambia mumewe. Mume akamwambia mkewe akubali tu, ila mwambie aje walale nyumbani kwake. Mume akazidi kumpa maagizo mkewe kwamba yeye atajificha uvunguni na upanga hivyo yule mwanaume akishavua nguo mwanamke atatakiwa kutoa ishara kwa kuning’iniza mkono kuelekea uvunguni ili mumewe auone kwa ajili ya kumfunza adabu mzinzi huyo.
Mdada akafuata masharti ya mumewe na hatimae wakaingia chumbani na yule bwana , mumewe akiwa tayari na upanga uvunguni mwa kitanda. Jamaa alipovua shati, mke alishangaa kuona ana makovu makubwa kifuani na mgongoni;
MKE: Heee mbona una makovu hivyo??
JAMAA: Niwe mkweli tu kwako dia!! Mie nina tatizo sana la kupenda wake za watu, waume wengi wamekuwa wakipanga kunifumania, nilishafumaniwa mara kumi na tisa, na wote walionifumania niliwaua. Ila jaribio la mwisho nilidakwa na mapolisi nikatumikia kifungo cha miaka 27 jela, Lakini ninavyopenda wake za watu sitaacha kuua. Hivi sina muda tangu nitoke huko jela hivyo nina ukame wa punda na nilipokuona moyo wangu ukakudondokea. Na nitatulia na wewe my dia.
MKE: Heee! Haiwezekani jamani!!
JAMAA: Sijamaliza dia, aliyesababisha nikamatwe na polisi ni yule mwanamke; alivyoona namwua mumewe akaamua kupiga simu polisi. Hata hivyo juzi juzi tu nilivyotoka nilimtafuta yule mwanamke na kumchinja kabisa!
MKE: Maweeeeeeee!
jamaa akaendelea kuvua nguo alipomaliza mdada akaanza kujitahidi kuning’iniza mkono ili mumewe atoke uvunguni aje kumuokoa, mume akabana kimya, kila mdada akijitihadi kupunga mkono hakupata jibu, Mdada akalalamika mpaka jamaa akamaliza shughuli zake akatokomea.
MKE: Huku akilia, ndio nini umenifanyia? Mbona hukutoka??
MUME: We we we……..! Weeeee mama naniii!!.. mwenyewe umesikia keshaua 19 ulitaka niwe wa ishirini?
**********





nmeipenda
duuuu!
duuh ni noumaa hata me nisingetoka !chezea kufa wewe!
SIKUBALI UJINGA KUMWAMBIA MKE WANGU ETI AKUBALI. ILA IKIWA HIVYO SITOKI UVUNGUNI NG’O KWANI SI ATAONDOKA NA ATAMWACHA KWANGU
Ooops mume hatari!