Home Vichekesho Mapenzi Na Pesa Ni Kulwa Na Doto Siku Hizi!

Mapenzi Na Pesa Ni Kulwa Na Doto Siku Hizi!

506
3

Hakika mapenzi na pesa ni mapacha wa damu siku hizi kwani inaonekana pesa ni sabuni ya roho na dawa ya penzi ni chapaa! Jamaa mmoja alimpigia simu mkewe kwa lengo la kumpa ujumbe na mazungumuzo yao yalikuwa kama ifuatavyo:

Mume: Hallo baby.

Mke: Hallo sweetie.


Mume: Leo nitachelewa kurudi nyumbani wangu!

Mke: Nishajua uko kwa wanawake zako, wewe ni malaya sana sijui ilikuwaje ukanioa. Nakuchukia kama nini sikupendi sikupendi sikupendiiiii!

Mume: Niko benki mke wangu.

Mke: Ahaaa! Sweetie, ulijuaje kama sina hela. Nitolee laki moja honey, nakupenda sana kuliko hata roho yangu. Nakutengea maji ya kuoga na ukirudi nakuogesha mwenyeweeee! Usisahau hizo pesa, ninunulie chips kuku baby! Mwaaaaaaaaaaaaaaah!

Mume: Ni benki ya kuchangia damu honey.

Mke: Nyoooooooooooooooo! Waambie wakutoe yote! ( Akakata simu)

**********





3 COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here