Mfungwa Ariel Castro aliyewateka nyara wanawake watatu na kuwafanya watumwa wa ngono kwa miongo miwili amepatikana akining’inia katika seli yake, gerezani huku nchini Marekani. Maafisa wanasema juhudi za kumuokoa hazikufaulu kwani alifariki kabla ya kufikishwa hospitalini.
Castro alikamatwa Mei baada ya mmoja wa wanawake hao kufaulu kutoroka na kuomba usaisidizi. Mwezi uliopita alikiri makosa yaliyojumuisha mashtaka zaidi ya mia tisa ya ubakaji, utekaji nyara na mauaji. Castro alihukumiwa kifungo cha maisha na tangu ahukumiwe alikuwa katumikia kifungo kwa muda wa wiki nne tu.
Castro aliyefariki akiwa na umri wa miaka 53 alikutwa na hatia ya makosa 937 kwa ujumla wake yaliyompelekea kifungo cha miaka 1000 jela sawa na kifungo cha maisha kwa kuwa si rahisi mtu kuishi miaka 1000! Hukumu yake hiyo ilitolewa Agosti 7 mwaka huu na alianza kutumikia kifungo hicho mara moja.
Castro aliwateka nyara Michelle Knight mwenye umri wa miaka 32, Amanda Berry mwenye umri wa miaka 27,Gina DeJesus mwenye umri wa miaka 23 mitaa ya Cleveland kati ya mwaka 2002 na 2004 kabla ya kuwahamishia nyumbani kwake na kuwafungia chini ya nyumba yake. Pia aliwalisha mlo mmoja kwa siku na walitumia ndoo za plastiki kwa ajili ya haja japo ilikuwa ni nadra sana kumwaga vinyesi vyao.
Castro alisikika mara kadhaa akijutia kitendo chake cha kuwateka wanawake hao na alikiri kwamba yeye si mtu mkorofi kama anavyoonekana ila amepata madhara makubwa yaliyompelekea kufanya kitendo hicho kutokana na kuangalia picha za ngono. Castro alikiri kwa kufanya makosa hayo kabla ya kuhukumiwa kifungo.
Chanzo: The Independent

I cant imagine jinsi hao wanawake walivyoteseka miaka yote hiyo.