Home Makala Huu Ni Ubaguzi Wa Rangi Au Ukweli? | Kauli Ngumu Za Kweli...

Huu Ni Ubaguzi Wa Rangi Au Ukweli? | Kauli Ngumu Za Kweli Ambazo Wengi HAwathubutu Kuzisema

446
0

Kuna kauli ni ngumu sana kuzizungumza hadharani kwa ujasiri mkubwa kama kauli iliyozungumzwa katika video hii! Nimewahi kujiuliza maswali mengi sana kuhusu Afrika! Kwa nini sisi Waafrika tunapigana wenyewe kwa wenyewe? Angalia Congo, Sudan,Somalia, Misri, Libya na kwingineko! Tanzania kumekuwa na harufu hiyo ya kutaka kupigana sisi kwa sisi hata kama utakuwa hutaki kulikubali hilo.

Na lugha inayotumika ni kusema kundi moja ni la Waasi wakipigana na serikali au kundi la Kigaidi! Inawezekana kabisa mauaji ya kimbari ya Rwanda hayajatufunza jambo kwani bado dunia inaruhusu watu wa jamii moja kupigana na kuuana kama wanyama! Ukiangalia filamu moja ya Attack in Darfur utaona jinsi wazungu walivyojaribu kubainisha na kutushangaa kwa kiasi fulani pale wanapoona Wasudan waarab (Janjawidi) wakiwaua Wasudani Weusi! Nanukuu sehemu ya filamu hiyo, “….Inashangaza kuuana wao kwa wao, ni sawa na wanyama wala nyama kuwaua wanyama wenzao….!”

Hakika ni jambo la kuhuzunisha sana na ukiweza tafuta filamu hiyo uone picha halisi ya Waafrika tunavyouana! Ipo pia filamu moja ya Bruce Wills yenyewe inaelezea mauaji ya DR Congo! Ni filamu ambazo ni ngumu sana kuziangalia! Pia mcheza filamu maarufu sana wa mchezo wa 24, Jack Bauer ameelezea pia katika moja ya filamu yake namna waafrika tunavyouana sisi kwa sisi na kutumia watoto wadogo kama askari wa vita! Wakati fulani hata majeshi ya kulinda amani yanapata wakati mgumu sana kupambana na hawa askari kwa sababu wengi ni watoto wadogo sana!


Maswali magumu yenye majibu rahisi ni haya, kwa nini tuuane wenyewe kwa wenyewe? Mbona sisikii nchi za Ulaya na Amerika zilizoendelea wakiuana wao kwa wao? Waafrika hatutengenezi silaha nzito za kivita, ni nani anawauzia wale wanaoitwa waasi? Wanazinunua ili wawaue kina nani? Tunatambua kuwa tunauana wenyewe kwa wenyewe wakati bara letu ni tajiri kiasi kwamba kila Mwaafrika ana nafasi ya kuishi kwa furaha? Haya ni maswali magumu yenye majibu mepesi!

Hebu tafakari maneno yaliyopo katika video hii halafu mjulishe na mwenzako!



LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here