Unaweza usiamini sana macho yako lakini huu ndio ukweli wa mambo. Mtu mrefu zaidi duniani anayeshikilia rekodi ya dunia Sultan Kosen, mwenye urefu wa futi 8 na inchi 1 kwa mara ya kwanza kakutanishwa na mtu mfupi zaidi anayeshikilia rekodi ya dunia ya Guinness He Pingping mwenye urefu wa futi 2 na inchi 5.
Watu hawa ndio wanaoshikilia kwa sasa rekodi za Guinness za dunia za mtu mfupi na mrefu ambao walikutanishwa jana. He Pingping ni mfupi sana kiasi kwamba mkono wake ni mdogo hauwezi kuzunguka kidole kimoja cha Kosen. Hivi ni vioja ambavyo kwa hakika unahitaji kuvishuhudia kwa macho yako mwenyewe!
