Home Vichekesho Gesi Ya Mtwara Yazua Balaa

Gesi Ya Mtwara Yazua Balaa

486
0

Bibi mmoja kutoka Mtwara alikuwa anasumbuliwa na tumbo kwa muda mrefu sana! Baada ya miaka kadhaa ya mateso huyo bibi, hivi majuzi tu alipata ushauri wa kwenda mhimbili ili akafanyiwe uchunguzi zaidi.

Alipofika akafanyiwa uchunguzi na haya yalikuwa ni mazungumuzo kati ya tabibu na huyo bibi,

Tabibu: Pole sana bibi, TUMBO LAKO LIMEJAA GESI itabidi upasuliwe ili itolewe.

Yule bibi kusikia hivyo akaruka juu na kukurupuka huku anapiga mayowe,

Bibi: Haiwezekani, hii ni gesi yangu na ninatafuta mwekezaji mimi mwenyewe. Hii haipelekwi Dar es Salaam ng’oooo! Kwa kweli tumejaliwa wana Mtwara, gesi baharini mpaka matumboni!

**********