Home Jamii Malala Aiasa Dunia Kupitia UN | Watoto Wa Kipakistani Kusoma Kwao Ni...

Malala Aiasa Dunia Kupitia UN | Watoto Wa Kipakistani Kusoma Kwao Ni Ndoto

448
0

Utamkumbuka binti mdogo Malala Yousafzai mwenye umri wa miaka 16 raia wa Pakistani aliyepigwa risasi na Talebani mwaka mmoja uliopita kwa kile walichodai kupinga watoto wa kike kusoma. Talebani wamekuwa wakiendesha kampeni ya kupinga watoto wa kike kusoma nchini Pakistani. Pakistani ni moja ya nchi masikini zaidi duniani. Watoto wengi katika nchi hii hawabahatiki kabisa kusoma hii ni kutokana na ukata wa kimaisha ambao huwapelekea kufanya kazi wakiwa wadogo sana ili kutengeneza vipato kwa ajili ya familia zao.

Pakistani imekuwa katika machafuko kwa muda mrefu na si jambo la ajabu raia wake kuwa na maisha duni. Lakini hili linalohusu elimu, nina amini kuna jambo la msingi linatakiwa kufanyia ili kuwakomboa watoto wa Pakistani. Mashirika kama Save Child na mengineyo yamekuwa yakijitahidi sana kupigania haki za watoto duniani lakini bado nguvu ya ziada inahitajika.

Malala alifanyia matibabu ya hali ya juu nchini Uingereza na sasa karejea katika hali yake ya kawaida na jana ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa ambayo aliiadhimisha kwa namana ya pekee pale baada ya kupata nafasi ya kuhutubia baraza la umoja wa mataifa.Malala amekuwa chachu kwa watoto wengine wa Kipakistani kukazia masuala ya elimu. Malala alipigwa risasi Oktoba 9, 2012 wakati basi lao la shule liliposhambuliwa na Watalebani. Malala ameeanza masomo yake tena nchini Uingereza na amependekezwa kuwania tuzo ya amani ya Nobel kama mwanaharakati anayehimiza mtoto wa kike kupata elimu.


Malala ameishangaza dunia pale aliposema, “….Watalebani wamenipiga kwa risasi kichwani kwangu, walidhani watatunyamazisha lakini wamefeli. Siwachukii watalebani. Hata leo hii nikiwa na bunduki mkononi mwangu na aliyenipiga akawa mbele yangu sitampiga kwa risasi….” haya ni baadhi ya maneno ambayo Malala aliyatamka katika mkutano huo wa umoja wa kimataifa.

Hii Hapa Ni Video Ya Malala

Malala aanzisha mapambano ya elimu kwa watoto wa kike Umoja wa Mataifa


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here