Madenge alikuwa anasafiri kutoka Kigoma akielekea Bukoba kwa basi na abiria wengine. Kwa bahati mbaya wakiwa njiani basi lao lilitekwa na majambazi. Majambazi waliwaamuru abiria watoe kila walichonacho na ambaye angekaidi wangemdunga sindano ambayo ilikuwa na damu ya mwenye Virusi Vya Ukimwi.
Watu wote wakatoa kila kitu walichonacho lakini Madenge hakutoa; wale majambazi wakamchoma na ile sindano. Baada ya kuachwa hawana kitu mmoja wa abiria alimwuliza madenge,
Abiria: Mbona wewe hujatoa vitu vyako na umekubali kuchomwa sindano yenye Ukimwi?
Madenge: Hawakujua kama nilikuwa nimevaa Kondomu!
**********



