Mwanafunzi mmoja alikuwa anatafuta namna ya kukwepa adhabu ya kutokufanya zoezi la fizikia ambalo mwali wake alilitoa darasani na mazungumuzo yao yalikuwa hivi;
Mwanafunzi: Eti, mwalimu?
Mwalimu: Unasemaje?
Mwanafunzi: Unaweza kuniadhibu kwa jambo ambalo sijalifanya?
Mwalimu: Hapana.
Mwanafunzi: Vizuri mwalimu, kwani sijafanya lile zoezi lako la jana!
**********



