Home Jamii Utoaji Mimba Ni Uuaji; Mimba 59,131,287 Hutolewa Kila Mwaka Duniani Kote!

Utoaji Mimba Ni Uuaji; Mimba 59,131,287 Hutolewa Kila Mwaka Duniani Kote!

398
0

Picha ya kichanga kilichotolewa kabla ya kuzaliwa

Je, umewahi kushiriki? Kina dada na kina mama wengi kote duniani wamekuwa wakitoa mimba kila uchao kwa visingizio mbalimbali. Kila mmoja wao amekuwa na sababu ambazo anaamini ni za msingi kabisa kwake kuweza kutoa mimba. Kwa namna moja au nyingine, utoaji mimba wa aina yoyote ile ni uuaji. Kama MUNGU alitujua tangu tu matumboni mwa mama zetu basi kuna kila sababu ya kuhakikisha uumbaji wake unaheshimiwa.
Zaidi ya mimba 59,131,287 salama kabisa hutolewa duniani kila mwaka! Kwa bahati mbaya ukubwa wa tatizo hili lipo katika nchi zinazoendelea. Hii ni kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa mwaka 2006 na inawezekana tatizo la utoaji mimba limeongezeka zaidi katika miaka ya hivi karibuni kutokana na mabadiliko makubwa ya kimaisha. Mgreth Sanger alisema, “Jambo la rehema zaidi ambalo familia inaweza kumfanyia mtoto mchanga aliyepo tumboni ni kumwuua!” Hii ni kutokana na ukweli kwamba hakuna mimba isiyo na familia!

Kutoa mimba ni dhambi kwa mtoto, ni dhambi kwa mama, ni dhambi kwa jamii na ni dhambi mbele za MUNGU! Sina jibu sahihi juu ya kuzuia tatizo la utoaji mimba lakini kila mmoja wetu akiwajibika kisheria na kwa sera nzuri zinazotekelezwa tunaweza kuzuia utoaji wa mimba. Ni mara ngapi umewahi kufurahia kuishi kwako? je, ingekuwa wapi hiyo furaha yako endapo mama yako angekutoa ukiwa bado ni mimba? je, unavyotoa mimba unafikiri unatoa kitu gani.
Utoaji mimba si jambo binafsi, kila mtu anaguswa na utoaji wa mimba. Hivyo ni wajibu wetu sisi sote kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili. Chukua muda wako uiangalie video hii mwanzo hadi mwisho mara nyingi uwezavyo halafu ujiulize umeshiriki mara ngapi kuwa mwuuaji!

Bofya Hapo Chini Kuangalia Video Hii

Tahadhari!!! Video Hii Inatisha na inafaa kwa watu wenye umri unaoanzia miaka 15

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here