Home Vichekesho “Ungekuwa Wewe Ungefanyaje Afande!!!!”

“Ungekuwa Wewe Ungefanyaje Afande!!!!”

1024
1

Dereva mmoja wa basi dogo la abiria alijikuta matatani mara baada ya kuwavaa watu 25 waliokuwa kando ya barabara maarufu sana iendayo Mbagala. Mkasa huu ulisababisha vifo vya watu wapatao 25 hivyo dereva hakuwa na ujanja wa kukwepa mkono wa sheria. Alipokamatwa na polisi na kuhojiwa, mahojiano yake na polisi yalikuwa hivi,


Trafiki: Ilikuwaje ukagonga watu wote hawa?

Dereva: Nilikuwa spidi sana ghafla nikaona kundi la watu wengi kushoto na mtu mmoja kulia, breki zikafeli na ndani nina vichwa kama 50 hivi, je unngekuwa ni wewe afande ungefanyaje?

Trafiki: Ningemgonga yule mmoja kuokoa wengi!

Dereva: Ehee! Ndivyo akili zangu zilivyonituma lakini yule mpumbavu mmoja alikimbilia kule kule kwa watu wengi akafikiri mimi chizi sijamwona, nikamfata kule kule ndio maana nikawapa kichapo wote!

Trafiki: Duh! Wewe nkaliiiiiiiiii!

**********

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here