Jamaa mmoja alikuwa katoka katika mihangaiko yake jua likiwa limekolea sana majira ya mchana na akalazimika kutafuta kivuli ili apate kupumuzika kidogo. Lengo lilikuwa kupisha jua kali lililokuwa linamwakia lipate kupungua kidogo.
Wakati amekaa chini ya mti wa mpera mawazo yakamjia. Akayaangalia yale mapera kisha akatafakari akijisema moyoni. Nimeamini Mungu amekuwa akikosea vitu vingi sana kuvitengeneza. Ona mti wote huu na ukubwa wake una vijimatunda vidogo dogo! Akaendelea kuwaza, halafu cha kushangaza maboga makubwa vile lakini miti yake inatambaa. Ningekuwa mimi; mpera ungekuwa na matunda kama boga na maboga yangekuwa na matunda kama mapera.
Wakati akitafakari hayo usingizi mzito ukampitia. Akiwa usingizini pera moja likadondoka na kumwangukia puani. Alijisikia maumivu na akashtuka. Baada ya kushtuka na kuona pera limempiga puani akajisema, kweli Mungu ni wa ajabu na hakika anakijua anachokifanya, hivi hili pera lingekuwa kama boga sasa hivi ningekuwa sina pua wala meno. Hakuna kama Mungu akainuka na kuendelea na safari zake.
Jumapili Njema!!!
**********




T
nomah kwel kwel!
Kweli Mungu ni Mkuu.
Huyo ni zuzu
hapo bado sijavunjika mbavu
kumbe unaakil ee..
i don thnk sooooooooooooo