Kwa kweli mimi nilipoangalia video hii nilicheka sana na ninaamini hata wewe utacheka tu. Kwa tafsiri rahisi kwa wale wasiojua Kikristu. Mwalimu alikuwa anafundisha moja ya somo linalohusiana na mambo ya taaluma mbalimbali za watu. Hivyo akalazimika kuwauliza wanafunzi wake taaluma ni kitu gani. Baadhi ya wanafunzi walielezea na kutoa jibu sahihi.
Mwalimu aliamua kuwauliza wanafunzi hao mmoja mmoja wanapenda kufanya kazi gani pindi watakapohitimu masomo yao. Kila mmoja alieleza dhamira yake ya kufanya kile anachokipenda. Wapo waliotaja kazi ya ualimu, uhandisi, utabibu, uuguzi na nyinginezo. Kuna mmoja alizua kasheshe darasani mara baada ya mwalimu kumwuliza yeye angependa kuwa nani akimaliza masomo yake, jibu lake lilikuwa ni vituko na ndilo lililonifanya nicheke sana!
Bofya Hapo Chini Kuona Video Yake



