Home Makala Ukijisikia Namna Hii Ujue Uko Katika Mapenzi | Sehemu Ya Pili |...

Ukijisikia Namna Hii Ujue Uko Katika Mapenzi | Sehemu Ya Pili | Makala

499
0

Huu ni mwendelezo wa makali hii inayozungumuzia namna ya kutambua mapenzi ya dhati! Endelea…

Ni vigumu kutambua penzi la kweli lakini ishara za penzi la kweli huwa zinaonekana kwa dhati iwapo mahusiano yako hayana mawaa! Penzi la dhati hujengeka lenyewe na huimarishwa na nguvu ya mvuto wa dhati toka moyoni! Huwezi kuwadanganya watu iwapo penzi la dhati limeota kwenye moyo wako hata ufanyej, kamwe huwezi kwa sababu penzi la dhati halilazimishwi!

Kama upo katika mahusiano ya kingono na unataka kutambua kwamba unachokifanya ni mapenzi au mihemko ya mwili tu; zipo ishara 12 zinaweza kukusaidia kutambua kama umezama katika dimbwi la mapenzi!

1.       Kutoa Na Kupokea Kwa Moyo Mweupe Wa Dhati

Ukitaka kutambua kuwa mtu uliye naye unampenda hebu jaribu jambo hili, ukitaka kumpa kitu chochote cha thamani mpenzi wako unajisikiaje? Je, unajisikia kumdai? Unajisikia kumnunua? Unajisikia fahari? Roho inakuuma sana?

lovegluelogo
Mapenzi Ya Dhati Hayanunuliwi

Kama unajisikia hali hii, hakika hauko katika mapenzi kwa sababu mapenzi ya dhati humfanya mtu asisikie kupungukiwa akitoa kwa ampendaye! Si nyie wenzangu na mimi mnahonga funguo badala ya gari, mkitibuana kidogo, “ Nipe funguo yangu!”

2.       Furaha Ya Dhati Na Kweli

Ukiwa katika mapenzi ya kweli wakati wote utajisikia mwenye furaha ukiwa pamoja na mwenza wako pasipo kujali matatizo au vikwazo vinavyokukabili. Hii ndio maana hata watu ambao wengi wetu huwa tunawadhania hawastahili kupendwa utaona wana wapenzi mfano walemavu, mafukara, wagonjwa na kadhalika kwa sababu wale wanao wapenda hawaoni udhaifu ambao wewe unaweza ukawa unauona!

3.       Maumivu, Wivu Na Hasira

Iwapo upo katika dimbwi la mapenzi, mpenzi wako anapokukosea unasikia maumivu, wivu au hasira lakini si ya kumfanya adhurike. Unajisikia kuumia kwa sababu unahisi umesalitiwa, unahisi amekupuuza, unahisi hakufikiria uwepo wako wakati anakukosea!

4.       Kujitoa Mhanga

Ukiwa katika dimbwi la mapenzi, uko tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya furaha au uzima wa mpenzi wako hata kama mpenzio hata tambua wala kuliona hilo!

5.       Matumizi Ya Nguvu, Jitihada Na Nyenzo Zote Kudumisha Pendo

Siku zote uko radhi kutumia nyenzo zote kwa gharama yoyote ili kumfanya mwenza wako ajue anapendwa na aendelee kukupenda.

6.       Huwezi Kumwumiza

Mara zote utajitahidi usimwumize mwili au moyo mpenzi wako, hata kama itatokea kuna jambo linalokuhusu ambalo akilijua litamwumiza roho una kuwa radhi kumficha maisha yake yote maana hutapenda kumwona anaemia!

7.       Kulipa Ahadi

Mara zote ukiwa katika mapenzi utajitahidi kulipa ahadi zote ambazo unakuwa unazitoa kwa mwenza wako hata kama umeamua kuvunja ahadi au makubaliano, utajikuta unalipa ahadi ili asikuone wewe mwongo au mwenye ahadi hewa. Hali hii ukiona inajitokeza kwako basi ujue upo katika dimbwi la amapenzi

8.       Kuendesha Maisha Katika Moyo Wa Mwenza Wako

Hiki ni moja ya vipengele vigumu sana maana vinahusiana na kujitoa mhanga. Mara nyingi utajikuta unaendesha maisha yako katika moyo wa mwenza wako hii ina maana kwa kila jambo ambalo utataka kulifanya ni lazima ufikirie lina faida au athari gani kwa mpenzi wako. Ni ukweli uliodhahiri kwamba hutakuwa radhi kufanya jambo litakalo uumiza moyo wake hivyo unajikuta unaendesha maisha yako katika moyo wa mwenza wako!


9.       ‘Kugawana Umasikini’

Utajikuta unakuwa tayari kubeba matatizo ya mpenzi wako hata kama hupaswi kufanya hivyo ili mradi uone unampunguzia matatizo ambayo wakati fulani humpasa kuyabeba kwa sababu anaweza akawa ameyatafuta mwenyewe au katengenezewa!

10.   Wivu Wa Majivuno

Inawezekana kabisa ukiwa na mtu mwingine katika ushindani wa jambo Fulani, unaweza kujisikia wivu wa hasira kwa sababu hukupenda ushindwe na hupendi kumwona mwingine anakushinda lakini inapotokea kwa ushindani ule ule anashinda mpenzi wako, unajisikia wivu wa majivuno! Una hisi hata wewe ni sehemu ya ushindi wake na unahisi umeshinda wewe!

11.   Kukubali Mateso

Haina tofauti sana na kujitoa mhango japo tofauti ni kwamba hapa unakuwa unakubali kuteseka ili umwone mwenza wako ni mwenye furaha.

12.   Kiherehere

Mara zote utajisikia kufanya jambo na kumfanyia mpenzi wako hata kabla hajaamua kufanya yeye mwenyewe. Kwa ufupi unakuwa na kiherehere mbele zake

Hizi ndizo ishara 12 ambazo zinaweza kukuthibitishia kuwa kwa hakika upo katika mapenzi!

**********

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here