
Katika mkoa mmoja ambao una watu wengi wa jamii ya wamasai wanaoishi kwa wingi na shughuli zao kubwa huwa ni ufugaji kulizuka dhoruba mara baada ya mwekezaji mmoja kuvamia kijiji kimoja ambacho wamasai wengi wanaishi.
Baada ya kufanya manyanga yake na serikali kama kawaida, mwekezaji huyo alipewa eneo na akaanza kuliweka alama na mipaka tayari kwa uwekezaji. Wamasai hao walipoona hilo wakakubaliana kuhakikisha mwekezaji huyo hachukui ardhi waliyodai kwamba ni yao.
Kila yule mwekezaji alipoanza kuendeleza miradi yake ya uwekezaji wamasai wakawa wanafanya uahribifu. Yule mwekezaji akaamua kuweka askari walinde lakini kwa bahati mbaya askari wengi walijeruhiwa vibaya wakakimbia. Kwa sababu pesa ina nguvu yule mwekezaji akakodi askari wakiwa na silaha nzito yakiwemo mabomu ya kutupa na mikono.
Timbwili likazuka mara baada ya wale askari kuvamia kijiji n ugomvi mkubwa ukazuka. Masai mmoja alipata fursa ya kumwona askari mmoja akiwa kazubaa na akaamua kumtupia mkuki! Yule askari kwa uhodari mkubwa aliudaka ule mkuki na kuukita chini mara baada ya kuudaka. Askari yule naye alipoona hali si shwari alichomoa bomu moja akamtupia yule masai na kwa bahati nzuri yule masai akalidaka lile bomu! Kwa kutaka kumwonyesha yule askari kwamba na yeye ni hodari mara baada ya kulidaka lile bomu, masai akalibamiza chini. Kilichotokea mimi sijui maana nilikimbia!
**********



