Kuna tabibu mmoja alikuwa anamfanyia upasuaje mgonjwa wake ambaye alikuwa na matatizo katika korodani (makende) yake. Tabibu aliamua kuzitoa kabisa korodani za mgonjwa wake na kuziweka kwenye kijisahani kwa lengo la kutafuta namna ya kurejesha uzima wa mgonjwa wake. Hii ni kutokana na umhimu wa viungo hivi katika uzazi!
Upasuaji ulianza vizuri kwa bahati mbaya mlango wa chumba cha upasuaji haukufungwa hivyo paka akaingia na kuzipitia zile korodani na kuzila. Tabibu alipatwa na woga wa kupoteza kazi yake hivyo akafikiri akaona suluhisho ni kumwekea viazi mgonjwa wake pasipo kumwambia.
Baada ya upasuaji mgonjwa aliruhusiwa. Siku kadhaa baadae tabibu alikutana na mgonjwa wake na haya yalikuwa ni mazungumuzo yao,
Tabibu: Unaendeleaje?
Mgonjwa: Nashukuru sijambo kabisa na ninaendelea vema, ila nina tatizo moja tu!
Tabibu: Lipi hilo?
Mgonjwa: Tangu unifanyie upasuaji nashangaa sana, badala ya kuota mavuzi naota MATEMBELE!!
**********



