Home Video Ni Kweli Tanzania Tumefikia Hapa??????

Ni Kweli Tanzania Tumefikia Hapa??????

427
0
2Q==
Masikini mtoto huyu! Picha ya kuhuzunisha ya mtoto akijaribu kuinuka baada ya kupigwa bomu katika mkutano wa CHADEMA! Inahuzunisha sana, hebu iangalie video yake hapo chini!

Tazama kwa makini sehemu hii ya video ili uhisi jinsi inavyoumiza!

 

Sina maelezo mazuri ya kuelezea hili tukio ila kwa ufupi hii ni video ya bomu lililoripuka Arusha hivi karibuni katika mkutano wa CHADEMA. Kuna maswali mengi ambayo hayana majibu na kwa hakika majibu yake yanatakiwa yapatikane. Wapo wanaodhani hizi ni mbinu chafu za Chama Tawala kuharibu mikutano ya CHADEMA  kwa lengo la kuwatia hofu wananchi ili wasiwe wanahudhuria kwa wingi kwenye mikutano yao! Je, ni nani mwenye kuthibitisha dhana hii? Mimi sifahamu na siwezi hukumu kwalo!

Wapo wanaosema hizi ni janja za CHADEMA  kuonyesha umma kuwa serikali imeshindwa kuongoza nchi na imekuwa ikiwaonea watu wanapojaribu kutafuta haki zao. Pia dhana hii hakuna wa kuithibitisha ma huwezi kumhukumu mtu kwa dhana hii!

Wapo wanaoamini kuna mkono wa mtu asiye na dola ila mwenye lengo la kuvuruga nchi kwa lengo la kuvuna utajiri uliogundulika siku za hivi karibuni wa gesi na madini ya urani iwapo nchi itakuwa machafukoni! Hii pia ni dhana ambayo nani anaweza kuithibitisha?

Hakika kwa hali hii si jambo zuri na ni ishara mbaya kwa nchi nzuri kama Tanzania. Ni busara na heri kwa mutu yeyote mwenye ushahidi wa namna yoyote ile auwasilishe kwenye vyombo vya dola ili wenzetu wasiendelee kupoteza maisha. Nani anajua, leo wamekufa wao kinyama na pengine kesho yanaweza yakakukuta wewe kwa namna iyo hiyo.

Tanzania ni nchi nzuri sana na tunahitaji kulinda uzuri wa Tanzania. hata kama mwenye misheni hii ananufaika kwa lolote lile ila atambue kwamba TANZANIA SALAMA KWANZA, PASIPO TANZANIA SALAMA HAKUNA ATAKAYEABUDU, HAKUNA ATAKAYEHUTUBIA MIKUTANO, HAKUNA ATAKAYEOMBA RIDHAA YA KUONGOZA WATU, HAKUNA ATAKAYEWASAIDIA WATANZANIA MASIKINI WANAOHITAJI MSAADA KUJIKWAMUA NA UMASIKINI WAO! TUMEKUWA TUKISIFIKA KWA KUFANYA SULUHU NA KUWA WAVUMILIVU KWA MAGUMU MENGI, BASI NA HILI TUKIO LIWE LA MWISHO KUTOKEA KATIKA UHAI WA TANZANIA NA WATANZANIA!

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA!

 

Bofya kifungo hiki kuangalia video hii: Hivi Ni Kweli Tanzania Tumefikia Huku?????

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here