
Mwalimu mmoja alikuwa anafundisha wanafunzi wa kidato cha pili. Ilikuwa ni kawaida yake kuandika notisi kwanza ubaoni na akimaliza anawaelezea wanafunzi maana ya kile anachokiandika.
Kwa bahati mbaya siku moja wakati anafundisha alijikuta akijamba. Kitendo kile kiliwafanya wale wanafunzi waangue kicheko kikubwa sana. Mwalimu akaona aibu akatoka darasani na akaenda kuomba likizo ya mwezi mmoja ili ile aibu ipite. Aliamini mwezi ukipita watakuwa wamesahau.
Baada ya mwezi yule mwalimu alirudi kufundisha tena, akiwa darasa lile lile aliwauliza wanafunzi wake;
Mwalimu: Hivi mara ya mwisho tuliishia wapi?
Wanafunzi: Pale ulipojamba.
Ikabidi yule mwalimu aache kazi kabisa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
**********



