Katika kitu kinachoaminika ni cha ajabu sana duniani ni muziki. Muziki umekuwa ukigusa hisia za watu na kuwafanya wajisikie faraja ya hali ya juu. Kuna wakati fulani inaaminika muziki umekuwa kama tiba kwa misongo ya mawazo na aina nyingine ya matatizo yanayofanana na hayo.
Jambo la kushangaza ni kwamba hata watoto wadogo wanaweza kuutambua muziki na kuutofautisha na kelele za aina nyingine. Hali hii inaweza kujidhihirisha kwani nimewahi kushuhudia mtoto mdogo ambaye hawezi hata kutembea ukimpigia midundo ya muziki anaanza kutikisa mikono na miguu huku akiachia tabasamu laini.
Angalia Video Hii Uone Kitu

