Saada Kilongo (26) siku ya mahafari yake mwaka jana 2012
Mfanyabiashara mrembo, Saada Kilongo (26), alipandishwa kizimbani mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana kushtakiwa kwa kukamatwa na madawa ya kulevya yenye thamani ya zaidi ya milioni 170/ -.
Akiwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Nyigulila Mwasebo, mshitakiwa hakuruhusiwa kujibu chochote, amerudishwa rumande hadi Julai 10, mwaka huu, wakati kesi yake itakaposomwa tena.
Wakili wa Serikali, Peter Maugo alidai kuwa Juni 24, mwaka huu, mtuhumiwa, mkazi wa Mbezi beach Rainbowalikamatwa akijaribu kusafirisha madawa ya kulevya aina ya efedrini HCL katika uwanja wa Julius Nyerere International Airport (JNIA). Mwendesha mashtaka alisema kuwa madawa hayo yalikuwa na thamani ya 170,481,000 /=
Swali ambalo huwa najiuliza kila siku, kama madawa ya kulevya ni haramu nani anayapangia bei? Kama yana bei basi yana soko na kama yana soko basi wanunuzi wanafahamika! Kweli madawa ya kulevya ni changamoto sana katika dunia hii!

