Home Vichekesho Mjini Mipango; Nguvu Kijijini Kwenu!!!!

Mjini Mipango; Nguvu Kijijini Kwenu!!!!

532
1

Jamaa mmoja alienda saluni moja maarufu sana ipo Kinondoni Manyanya kwa ajili ya huduma ya kunyolewa akiwa na mtoto.  Alipomaliza kunyoa nywele na ndevu akamwambia kinyozi amnyoe na yule mtoto ambaye alikuwa peku hana viatu. Yule jamaa bila hiana akatoka ili akamtafutie yule mtoto viatu na kumwacha akinyolewa. Hivyo ndivyo alivyomweleza kinyozi kwamba anaenda kumchukullia viatu mtoto dukani mara moja!


Yule kinyozi alikuwa kamaliza kumnyoa yule mtoto baada ya dakika kama ishirini hivi! Baada ya kusubiri kwa takribani saa tatu, yule kinyozi akaamua kuvunja ukimya.

Kinyozi: Oyaa! baba yako yuko wapi????

Mtoto: Yule sio baba yangu, kanikuta hapo nje nacheza kasema tuje wote tunyoe nywele!

Kinyozi: Duh! Nishaliwa!

**********

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here