Mayai Ya Kuku
Mama mmoja alikuwa anafanya usafi chumbani na ghafla kwa mara ya kwanza akakutana na kisanduku chini ya uvungu. Alipokifungua akakuta mayai 5 na shilingi milioni 1.Aliporudi mumewe akamuuliza,
Mke: Kisanduku hiki ni cha nini pamoja na haya mayai?
Mume: Kweli wataka kujua mke wangu?
Mke: Kwani siku hizi tunafichana!!
Mume: Tangu nimekuoa miaka mitano iliyopita nilijiwekea utaratibu kama nitatoka nje ya ndoa nanunua yai moja na kuliweka humu ndani ya kisanduku.
Mke: (Huku akifurahi) Kumbe mume wangu umetoka nje ya ndoa mara 5 tu tangu tuoane miaka 5 iliyopita?Waliokuwa wanasema wewe mhuni ni wachonganishi tu. Na vipi kuhusu hizo milioni 1?!
Mume: Huwa nayauza mayai pindi yanapokuwa mengi na pesa naziweka humo!
Mke akadondoka chini na kuzimia….!




