
SIku moja Massawe alienda baa kupata moja baridi na moja moto. Akiwa huko, akatokea bonge la mtoto wa kike ambaye kwa mtazamo tu alikuwa anaonyesha ni mtoto wa familia bora au jimama lenye uwezo wake!
Massawe akatupia ndoana mtoto kweli akanasa! Baada ya mazungumuzo ya kina yule demu akasema yeye ana kila kitu katika maisha yake ila kwa sasa anataka mume na moyo wake umemwangukia Massawe! Hii ilikuwa ni habari njema kwa Massawe.
Baada ya muda kupita yule demu alimtaka Massawe aongozane naye kwenda kwake! Walipofika kwake moja kwa moja wakavutana mpaka chumbani! Kwa kuwa yule demu alikuwa amekolea kwa Massawe akamwambia,
Demu: Baby, nifunge kamba hapa kitandani kisha unifanyie kitu chochote upendacho!
Massawe akachukua kamba na kumfunga vizuri kabisa pale kitandani kisha akakusanya kila alichokiona kina thamani kwake, Flat Screen Samsung 45″, simu, pesa ilikuwa kwenye droo takribani milioni sita na vingine vingi alivyoona vina thamani kisha akatokomea! Chezea kina Massawe weweeeeeee! Pesa kwanza!
*********




Haichekeshi
Haichekesh kabsa jpange upya
Nikweli