Sharobaro mmoja alipokea sms tatu kwa mkupuo na zilikuja na ujumbe huu; meseji ya kwanza ilitokea kwa mama yake na ilikuwa inasema hivi,
“Njoo utoe vyombo halafu ukaoshe, wageni wamemaliza kula. “
Meseji ya pili ilitoka kwa demu wake na ilikuwa inasema hivi;
“Mpenzi nataka Tsh 150,000/= nikafanye shopping ya sikukuu hii, jitahidi niipate….love you”
Na meseji ya tatu ilitoka kwa mshikaji wake,
“Jamaa yangu mbona unazingua? Mbona hurudishi nguo na viatu vyangu sasa hivi ni wiki ya pili au nije nikuvue kwa nguvu?”
Acha Usharobarooooooooooooooooooooo dogoooooooooooooooooo Fanya maisha!!! Hapa Kazi Tu




