Kuwa Zuzu Mzigo
Jamaa mmoja alikuwa anatembea nyuma ya zuzu fulani. Mbele yao kulikuwa na noti ya shilingi elfu kumi chini. Mambo yalikuwa hivi:
ZUZU: Asante Mungu nimeokota elfu kumi!
JAMAA: Halo bro, hicho ulichookota ni kitambulisho changu tafadhari nakiomba.
ZUZU: Hata kama mimi chizi, ila si mjinga kiasi hicho! Hebu niambie jina lako nani?
JAMAA: Jina langu Benki Kuu Ya Tanzania.
ZUZU: Mh! Haya, una umri gani?
JAMAA: Umri wangu Ni Shilingi Elfu Kumi
ZUZU: Dah! Kweli aise, kumbe kitambulisho ni chako! Nisamehe kwa kutokuamini Braza!!!





aaaaaaaaaaa
ayaaaaa
aaas