Home Mbavu Zangu Kichaa na mkojo

Kichaa na mkojo

905
0

 

Katika hospitali moja ya vichaa ilikuwa ni kawaida kwa nyakati fulani kuwapandisha wale vichaa juu kabisa ya ghorofa kwa kuwatoa katika vyumba vyao ili wapunge upepo kwa sababu hakukuwa na eneo la wazi la chini la kuwaweka. Jambo hili lilikuwa linafanyika kila siku na siku moja wale vichaa wakasimama kwenye kingo za jingo na kukojoa mkojo uliokuwa unatiririka chini kabisa ya jengo.

Kitendo hicho walikuwa wanakifurahia na kiliwapelekea wawe wanakifanya mara kwa mara. Wakati wakiendelea kushindana kukojoa kwa zamu kila mara, kuna kichaa mmoja wakati anakojoa ghafla alikatisha mkojo wake alipoona watu wanapita chini ya ghorofa. Mganga aliyekuwa anawauguza alipoona akajua mgonjwa wake anapata akili na kahisi si vyema kwanza kuwakojolewa watu na pia alikuwa anaona aibu kuchunguliwa akiwa anakojoa.

Kwa kutaka kuthibitisha hilo, mganga alimpima mgonjwa wake. Na mazungumuzo yao yalikuwa hivi,

Mganga: Mbona umeacha kukojoa ghafla ulipoona watu?

Kichaa: Niliogopa wasija wakaukamata mkojo wangu na kuuvuta nianguke!

Mganga akachoka!

**********