Ni utamaduni uliozoeleka kabisa kuona inapotokea askari amefariki dunia basi askari wenzake humsindikiza kwa kupiga mizinga kadha wa kadha au kupiga risasi kama ishara ya kutoa heshima na kutoa mkono wa buriani kwa marehemu! Wakati huu huwa ni wakati mgumu sana kwa kuwa siku zote kifo hakizoeleki.
Lakini pia ni utaratibu wa kawaida kabisa anapofariki dunia mwanamuziki basi watu hupiga nyimbo mbalimbali alizowahi kuziimba kama ishara ya kukumbuka na kumuaga marehemu. Hakika muziki una nguvu sana katika hisia za mwanadamu na hakuna wakati mgumu kama huu hasa pale unapokumbuka nyimbo alizowahi kuziimba marehemu!
Taratibu zote hizi Madenge alikuwa anazijua baada ya kushuhudia mazishi na askari kadhaa na baadhi ya wanamuziki. Lakini kuna jambo moja ambalo lilikuwa linamtatiza sana Madenge kila alipobahatiki mara mbili kuhudhuria mazishi ya walimu wake ambao walifariki kwa nyakati tofauti tofauti. Safari hii alikuwa ni mwalimu wa tatu kufariki katika shule yake na huyo mwalimu alikuwa ni rafiki kipenzi wa baba yake na Madenge hivyo alikuwa na kila sababu ya kuhudhuria mazishi!
Wakati Madenge anarejea nyumbani aliona hiyo ndiyo fursa pekee ya kumwuliza baba yake kile kinachomtatiza;
Madenge: Baba!
Baba: Naam.
Madenge: Nina swali linanisumbua sana kichwa!
Baba: Ushaanza ujinga wako.
Madenge: Kwani ushajua nataka kuuliza nini baba?
Baba: Hebu uliza haraka.
Madenge: Akifa mwanajeshi wanapiga risasi hewani, akifa mwanamuziki wanapiga nyimbo zake hii yote ni ishara ya kumuaga!
Baba: Haswaaaaa huo ni utaratibu uliozoeleka!
Madenge: Lakini kuna kitu kimoja sikielewe kwa nini akifa mwalimu hawamsindikizi kwa viboko? Maana siku zote mwalimu na kiboko. Na ingekuwa hivyo huyu mwalimu tuliyemzika leo ningemchapa kweli viboko, alikuwa anachapa kwa sifaaaaaaaaaaaa!
Baba: Hapa toto sina!
**********




mmh.!