Nani asiyejua ugumu wa kupata ajira sasa hivi hapa Tanzania? Inawezekana wewe hujui kwa sababu umelamba kitengo mahala fulani lakini kwa hakika mambo si shwari kabisaaaaa! Kama ni mwanamke ujue ni lazima watoa ajira watataka kukuvua chupi na kama ni mwanaume ujue jasho lako litaliwa na wanaume kilainiiii!
Ni jambo la kusononesha kabisa kuona mtu anataka ummpe % ya mshahara wako wakati hata uhakika wa kupata hiyo kazi bado huna. Amini usiamini hakuna wakati ulio mgumu kama wakati wa kusaka ajira. Kipindi hiki huwa kina stress nyingi sana na wakati fulani akili ya mtu huwa haikai sawa kabisa na anaweza akajikuta anakubali kila kitu ili apate kazi.
Tatizo liko hapa, wewe ukikataa mwenzako anakubali na ukisema ushitaki ni vigumu sana kupata ushahidi wa kutosha kumtia mtu hatiani. Soma hii meseji utanielewa tu hata kama huelewi!
**********



