Niliwahi kuuliza picha hii ni ya nani (Picha hiyo hapo juu) lakini hakuna mtu aliyeweza kutoa jibu na ikaishia hapo hapo. Najua wengi mnamfahamu Robert Nesta Marley maarufu kama Bob aidha kwa kusimuliwa au kwa kusikia nyimbo zake maana Tangu kifo chake hapajatokea mtu anapiga nyimbo za rege kama alivyofanya Bob marley!
Kulikuwa na hadithi nyingi sana juu ya kifo cha Bob na hakika watu wamekuwa wakijua mengi kulingana na wingi wa majarida kuandika habari zake. Kevin Macdonald ni mwongozaji wa filamu aliyeitende haki filamu hii ya Bob inayoelezea kwa undani sana maisha yake. Kwa mara ya kwanza nilipoona filamu hii sijaacha kuirudia tena na tena na nimegundua nguvu ya kipekee sana aliyokuwa nayo Bob.
Sio kwamba nakosea, nina kuhakikishia kabisa kama hupendi filamu jitahidi uiangalie hii hata mara moja tu na kama hujui kizungu, mtafute rafiki yako hata kwa ujira kidogo akupe tafsiri ya kila neno lililozungumuzwa katika filamu hii! Hakika hii ni filamu ya mwaka. Kutokana na kukua kwa maendeleo ya Kisayansi, filamu hii unaweza kuiangalia hapa hapa vunja mbavu! Kazi Kwako!


