Jamaa mmoja aliyejizolea umaarufu sana katika maeneo fulani ya Magomeni Mapipa jijini Daslam kwa kuwamudu wake zake watatu alizua kali ya mwaka siku chache kabla ya mfungo kuanza. Kutokana na ukweli kwamba dini ya jamaa huyu ilikuwa inamruhusu kuoa mpaka wake wanne na si kuishia kuwa na nyumba ndogo, bila hiana akaamua kuvuta mke wa nne, kitoto kibichi cha Kisomali ili mfungo wake uwe swadakta kabisa!
Mkewe mkubwa yaani mke wake wa kwanza aliulalamikia sana uamuzi huo na akaamua kulizua varangati. Wadukuzi wetu waliunasa mchezo mzima kwani bila hiyana katikati ya swaumu kali yule mama aliamua kumvaa mume wake,
Bi Mkubwa: Hivi wewe baba Havijawa wajiona kidume kweli? Umeniletea mke wa kwanza nikavumilia, ukaleta wa pili nikakaa kimya, ukaniletea wa tatu nikajifanya bwege! Sasa hivi umeamua kuniletea kitoto kidogo kabisa eti mke mwenza!
Mume: Kwani kuna ubaya mke wangu?
Bi Mkubwa: Huoni huo ubaya? Kinachoniuma zaidi yaani haijatosha kuokota hao wanawake na kuniletea hapa, umeamua kutulaza wote kitata kimoja! Mimi wa kulazwa kitanda kimoja na huyo wamwita mkeo, kitoto kidogo bado chanuka maziwa ya mamaye!
Mume: Haya ndio mapenzi shirikishi mke wangu, mbona hivyoooooo!
**********



