Siku za hivi karibuni Steve Kulialia alinaswa na kituo kimoja cha luninga cha Kenya akihojiwa ni kwa jinsi gani amekuwa akilia kwa ajili ya timu yake. Video ya Steve ya kuililia Yanga siku ilipofungwa goli 5 na Simba ilizagaa sana kwenye mitandao jambo lililokipelekea kituo cha luninga cha nchini Kenya kuja Tanzania kumtafuta Steve!
Mbali na maelezo mengi ambayo aliyatoa Steve aliamua kufunguka na kudai kuwa anapenda kuwa na mke wa Kikenya kwa sababu anawapenda sana wanawake kutoka Kenya! Vunja mbavu tumeamua kumpa taarifa Steve ajipange sana kuoa Mamanzi wa Kinairobi kwa sababu yatamkuta haya yaliyomo kwenye hii picha kama asipokuwa mwangalifu. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mamanzi wa Kikenya wanajua Kung fu, judo, karate na masumbwi! Jipange chali yangu!
**********

dah hii ni hatari kaka kazi na kichapo tudai haki za wanaume sasa.