Ushawahi kulisikia tangazo hili? Bila shaka ushalisikia, watonyaji wetu wanasema kwamba tangazo hili lilibuniwa kutokana na mkasa mmoja uliotokea maeneo ya Temeke!
Nafikiri wengi mnafahamu kwamba kuna sababu za kisayansi zinazothibitisha kuwa mwanaume aliyekatwa govi anapunguza hatari ya kuambukizwa VVU.
Jamaa mmoja huko Temeke aliamua kumpeleka ndugu yake ambaye alikuwa kafikisha umri wa miaka 25 lakini kwa bahati mbaya alikuwa hajatahiriwa. Kwa kuwa jamaa huyo alikuwa ameusikia huo ujumbe kupitia taarifa mbalimbali za kuelimisha rika ilimlazimu kuupenyeza huo ujumbe kwa ndugu yake ili amnusuru na janga hili.
Kutokana na jinsi alivyokuwa anamjua ndugu yake aliona si vema akimwambia kuwa anatakiwa kufanyiwa tohara hivyo aliamua kumdanganya kwamba anapaswa kufanyiwa uchunguzi wa kiafya kwani anataka wasafiri naye waende nje ya nchi. Yule jamaa alikubali na akaingizwa chumba cha uchunguzi.
Katikati ya uchunguzi daktari akaamua kuleta visu na mikasi kwa ajiri ya tohara. Kwa bahati mbaya yule jamaa aliviona na ikabidi ahoji:
Jamaa: Dokta, hivyo vyote ni vya kunipimia mimi!!!!????
Dokta: Ndiyo, safari yako ni muhimu sana, nchi unayoenda hii nyama huwa hawaitaki kwa hiyo nakukata kidogo hii nyama ili nifanikishe safari yako!
Jamaa: ( Akaruka toka kitandani na kupayuka huku anakimbia) Hakatwi mtu hapaaaaaaaaaaaa!
**********




Hahahaha ni nouma!